Maombi ya Kila Siku
“Kile ambacho moyo wako umekishikilia kinaweza kukukamata kwa urahisi. Tunaposhikilia Neno la Mungu mioyoni mwetu, hugeuka kuwa ngome yetu.”
Katika mzunguko wa shughuli za kila siku, tunapataje wasaa wa kutunza maisha yetu ya kiroho? Pamoja na nguvu nyingi kinzani zinazopigania usikivu wetu, ni muhimu zaidi kuliko hapo awali kutumia muda bora kila siku katika Neno Hai la Mungu – chanzo kimoja cha ukweli na uthabiti tunachoweza kukitegemea kila wakati! Kama vile Mathayo 24:35 inavyosema, “Mbingu na dunia zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.” Unaposoma machapisho haya yenye mwongozo juu ya kujitoa kwa Mungu kutoka kwa Timu ya God’s Heart TV, tunaomba kwamba Mungu afungue moyo wako kwa hekima Yake na kukusaidia kuona maisha kwa udhahiri – kupitia macho Yake.
MATOKEO YA KUTAMANI
Luka 12:15, “Akawaambia, ‘Jihadharini na kutamani, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu alivyo navyo.’” Watu wa Mungu, tunaishi katika ulimwengu ambapo wengi huamini udanganyifu muovu wamba uzima kweli umo katika wingi wa mali zao. Kama ilivyokuwa, ndivyo ilivyo. Ndiyo maana Bwana wetu Yesu Kristo alionya dhidi ya dhambi ya kutamani – tamaa ya kimwili ya kitu ambacho ni cha mtu mwingine inayokuangusha kwenye njia tupu ya kutoridhika. Kinachotupeleka hapo ni mtego wa kujilinganisha – huchochea kutamani, hivyo…
LINDA KILE AMBACHO SHETANI HAWEZI KUGUSA
1 Yohana 2:15-17, “Msiipende dunia wala mambo yaliyomo duniani. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake. Maana kila kilichomo duniani - tamaa ya mwili, tamaa ya macho, na kiburi cha uzima - hakitokani na Baba bali hutokana na dunia. Na dunia inapita pamoja na tamaa zake; bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu hukaa milele.” Watu wa Mungu, fikirini kile kinachowatia wasiwasi au kuwashughulisha sana. Tukijifunga kupita kiasi kwa mambo ya dunia hii, tunalemewa nayo. Usijifunge sana kwa kitu ambacho…
HATARI YA KUSHIKAMANA KUSIKOFAA
1 Wakorintho 7:29-31, “Nikisema hivyo ndugu zangu, nina maana kwamba muda uliobaki ni mfupi. Tangu sasa waliooa waishi kama hawakuoa; 30 na wana oomboleza kama hawaoombolezi; wenye furaha kama hawana furaha; wanaonunua kama walivyonunua si mali yao; 31 na wanaoshughulika na vitu vya dunia hii, kama hawahusiki navyo. Kwa maana dunia hii kama tunavyoiona sasa inatoweka.” Tunamshukuru Mungu kwa wingi wa rehema zake ambazo tumezipata katika mwaka unaoisha, na tunaamini unatarajia kuona utimilifu wa kile ambacho Mungu ameweka moyoni mwako…