Maombi Shirikishi

“Mapungufu yetu hayapunguzi mamlaka ya Mungu. Mapungufu yetu hayapunguzi uwezo wa mkono Wake wenye nguvu kutufikia. Upungufu wetu haumfanyi Yeye kutotosheleza.”

Maombi Shirikishi ni fursa ya kupokea maombi mtandaoni moja kwa moja kutoka kwa Ndugu Chris popote ulipo ulimwenguni kupitia Zoom. Maandiko yamejaa mifano inayoonyesha kwamba Mungu hazuiliwi na vizuizi vya wanadamu kama vile umbali. Kwa mfano, katika Mathayo 8:8, Akida wa Kirumi alimwambia Yesu, “Sema Neno na mtumishi wangu atapona” – na muujiza ulifanyika mara moja!

Ikiwa ungependa kuwa sehemu ya Huduma ya Maombi ya Pamoja kupitia Zoom, tafadhali jaza fomu iliyopo hapa chini na usubiri kwa subira jibu la barua pepe kutoka timu yetu kupitia info@godsheart.tv. Maombi haya yanatolewa bure. Kama Yesu Kristo alivyosema katika Mathayo 10:8 – “Mmepokea bure; toeni bure.”

(Tafadhali kumbuka kuwa kujiunga na Huduma ya Maombi Shirikishi kwenye Zoom kunahusisha kuonekana na kurekodiwa kupitia video, ambayo tunaelewa kuwa inaweza kuwa haifai kwa kila mtu. Unaweza pia kutuma ombi la maombezi jumuishi hapa.)

Soma ushuhuda wa wale waliojiunga na Maombi Shirikishi

UKOMBOZI KUTOKA KWA MAWAZO YA KUJITIA KITANZI NA UNYOGOVU!

No Comments

“Nawasalimu nyote katika jina la Yesu Kristo. Jina langu ni Mwaka kutoka Zambia na ningetaka kushuhudia wema wa bwana wetu, Yesu Kristo. Mwezi Januari 2024 nilianza kujihisi mnyonge mwilini na sikuwa na hamu ya kula. Baadaye mwezi wa Mechi, nilikuwa na uzito moyoni mwangu, na nilikuwa na huzuni tele na…

Soma Zaidi »

NDUGU CHRIS ALIPOOMBA, NILIPONA PAPO HAPO!

No Comments

“Jina langu ni Saimone kutoka New Zealand. Amani ya Mungu iwe nawe Ndugu Chris na nawatakia mwaka mpya wa baraka 2026 nyinyi wote katika God’s Heart TV. Nataka kutoa ushuhuda kuhusu kupona kwangu katika jicho langu la kulia papo hapo baada ya kuhudhuria ibada ya Maombi ya Ushirika kupitia zoom…

Soma Zaidi »